Ushairi ni utungo wa kisanaa unaotumia lugha teule na mpangilio fulani wa maneno badala ya kutumia lugha natharia(mflulizo).
Ushairi unaweza kuwa kipera cha fasihi simulizi (nyimbo) na pia katika fasihi andishi kwa sababu mashairi yanaweza kuwasilishwa kwa njia ya kukariri na pia kwa njia ya maandishi. Mashairi yanayoghanwa badala ya kuimbwa huitwa maghani.
Uchambuzi
Katika ushairi, tutaangalia:
Istilahi za Kishairi
Haya ni baadhi ya maneno ambayo hautakosa kukutana nayo unapozingatia ushairi. Ni muhimu mwanafunzi kuyajua vizuri.
- Shairi - ni sanaa ya maneno (utunzi maalum wa lugha ya kisanaa) unaotumia mpangilio na uteuzi maalum wa maneno na sauti ili kupitisha ujumbe fulani.
- Vina - ni silabi za mwisho katika kila kipande.
- Mizani - ni idadi ya silabi katika kila mshororo.
- Mshororo - ni msitari mmoja wa maneno katika shairi.
- Ubeti - ni kifungu cha mishororo kadhaa.
- Vipande - ni visehemu vya mshororo vilivyogawanywa kwa alama ya kituo(,)
- Ukwapi- kipande cha kwanza katika mshororo
- Mwandamo - Kipande cha tatu katika mshororo
- Ukingo - kipande cha nne katika mshororo
- Utao - kipande cha pili katika mshororo
- Mwanzo - mshororo wa kwanza katika ubeti
- Mloto - mshororo wa pili katika ubeti
- Kimalizio/Kiishio - mshororo wa mwisho katika ubeti usiorudiwarudiwa katika kila ubeti.
|
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni